Ranieri hakustahili kabisa kufukuzwa kazi




Olle Bergdahl Mjengwa 


SOKA ni mchezo wenye vitu vinavyobadilika haraka. Wakati huu msimu uliopita Leicester City iliongoza Ligi Kuu ya England.
Leo hii Leicester City imeshika nafasi ya 18 huku timu hiyo ikiwa katika nafasi ya kushika mkia.
Ni hali hii ambayo imeisababisha Bodi ya Leicester kumfukuza kazi Kocha Claudio Ranieri.
Kocha ambaye miezi mitatu iliyopita alipewa tuzo ya Kocha Bora wa Dunia kwa mwaka 2016.
Kocha ambaye aliwapa Leicester taji la Ligi Kuu kwa mara ya kwanza katika historia ya timu hiyo.
Dunia ya soka imeshangaa kuona jinsi Leicester imeshindwa kupata matokeo mazuri msimu huu. Lakini, mashabiki wengi wa soka pia wameshangaa sana kwamba Kocha Ranieri amefukuzwa kazi.
Bila shaka, Leicester ipo katika hatari ya kushuka daraja. Ipo katika hali mbaya sana kisoka huku wachezaji tegemeo kama Riyaz Mahrez na Jamie Vardy hawapo kileleni kama msimu uliopita.
Bodi ya Leicester inaamini kwamba Kocha Ranieri hana uwezo wa kuhakikisha Leicester mkataba mpya katika Ligi Kuu.
Na ukweli ni kwamba klabu nyingi zilivyo katika hatari ya kushuka daraja zinafanya vizuri zaidi zinapopata kocha mpya.
Kisaikolojia wachezaji wengi wanaona uteuzi wa kocha mpya kama mwanzo mpya wa timu yao na hivyo wanajituma zaidi.
Msimu huu tumeshaona klabu kama Crystal Palace, Hull City na Swansea City wakifukuza makocha wao, huku wakiamini kwamba kocha mpya ataweza kurudisha timu zao katika hali nzuri kimpira.
Hakika Swansea imeanza kucheza vizuri zaidi chini ya kocha wake mpya, Paul Clement na Hull City imekuwa katika hali nzuri zaidi tangu Marco Silva alipopewa kibarua na klabu hiyo.

Related

michezo na burudani 2186851990092653484

Post a Comment

emo-but-icon

item
Kicbjamii