Straika wa Serengeti afuzu Etoile



Mshambuliaji Yohana Mkomola 

MSHAMBULIAJI Yohana Mkomola aliyeenda kufanya majaribio klabu ya Etoile du Sahel ya Tunisia amefaulu, ila kwa sasa amerudi kwa ajili ya kujiunga na timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 17 ‘Serengeti Boys’ inayotarajiwa kwenda katika fainali za Vijana za Afrika.
Mkomola alijiunga na Etoile kwa majaribio ya siku 15 na atarudi kwa mara nyingine ili kuendelezwa na ataingia mkataba rasmi pale atakapofikisha miaka 18.
Mshambuliaji huyo aliyepata shavu hilo baada ya kufanya vizuri katika mechi tofauti za timu ya taifa ya vijana na Azam aliyokuwa anaichezea alisema, amejifunza mengi kwa kipindi hicho kifupi.
“Kwa siku hizo chache nilizokaa pale, nimejifunza mengi lakini nataka kujifunza zaidi, natarajia kujiunga nao tena,’’ alisema.

Related

michezo na burudani 4745466098438668223

Post a Comment

emo-but-icon

item
Kicbjamii