Huko kwenye filamu za Kibongo hakukaliki





FILAMU za Kibongo kwa sasa zimedorora sana. Takriban miaka miwili hali ya soko la filamu hizo imekuwa ikisuasua, lakini kwa 2017 limedorora kwa kiwango kikubwa kiasi kwamba hata wasanii wake wanaishi kwa kubangaiza.
Kipato kupitia tasnia hiyo kimekuwa muhali, kiasi cha kuleta mashaka makubwa kwa baadhi ya wasanii wakiamua kubadilisha upepo ili kupisha jinamizi lililopo sasa lipite kabla ya kurejea mambo yakiwa shwari.
Kumekuwa na mitazamo tofauti juu ya hali hiyo, wanunuzi wa kazi hizo na hata wasambazaji kila mmoja amekuwa na hoja zake kubwa ikielezwa kifo cha nyota wa zamani wa fani hiyo, Steven Kanumba ni tatizo lililochangia kuzika filamu. Wanadai kifo chake kimechangia kushusha soko la filamu za Kibongo wakiamini kama angekuwa bado yu hai angeendeleza moto wake wa kuitangaza tasnia hiyo nje ya nchi kama alivyofanya na kuipaisha kimataifa.
Kanumba alifariki mwaka 2012 ambapo kila sinema kwa wakati huo ilikuwa ikiuza tofauti ilikuwa ni uuzaji wa nakala nyingi tu huyo ameuza nakala kadhaa na yule kamzidi kwa kuuza nyingi lakini wadau wa filamu wanasema kuwa tangu filamu na muziki virasimishwe hali ni mbaya kwa watu wa filamu.
Mwanaspoti limefanya utafiti mdogo kubaini kudodora kwa soko la filamu Bongo, kuna mambo kadhaa yaliyolifikisha soko la filamu kushuka, ikiwa kiuchumi, ubora wa kazi, Tafsiri ya sinema za nje, wauzaji wa kazi za nje na kutegemea wafanya maamuzi kuwa sehemu moja yaani Kariakoo.

KIUCHUMI
Kwa sasa hali ya kiuchumi kwa wapenzi wa filamu ambao sehemu kubwa ni wale waliojiajiri haipo sawa hivyo si rahisi sana mtu kununua filamu moja kwa kiasi cha Tshs. 3,500 wakati akitoa Tshs. 700 hadi 1,000 anapata tamthilia yenye sehemu nyingi kuliko filamu moja tena iliyogawanywa mara mbili.
Hali hiyo imewafanya watengenezaji wa filamu za ndani kujikuta wanakosa wateja wa kununua kazi zao ambazo zinaonekana ni gharama kuliko zile za kutoka nje ambazo zinauzwa kwa bei nafuu zaidi lakini huku zikiwa zimesheheni ustadi mkubwa kwa kila Nyanja.
Wasambazaji wa ndani wanalalamika kuwa ushindani haupo sawa kwani sababu inayowafanya wao wauze bei kubwa ni kulingana na uwepo wa kodi lukuki na taratibu za kisheria ambazo wale wauzaji wa filamu za nje hawawajibiki nalo, sinema zao hazikaguliwi, hazilipiwi kwenye Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na kupewa Stempu zinazotambulisha mlipa kodi katika sinema.
“Sisi tunabanwa kodi ni nyingi sana nikienda Cosota nalipia, baada ya hapo nakwenda Bodi ya Filamu kukagua sinema yangu nalipia kwa kila dakika 1,000 nitokea hapo naenda TRA nanunua Stempu nitauza Dvd 700?,” anauliza Athuman msambazaji.


Related

michezo na burudani 4050128222779812457

Post a Comment

emo-but-icon

item
Kicbjamii