Serengeti kuidhamini Taifa Stars
http://maisharaisi.blogspot.com/2017/05/serengeti-kuidhamini-taifa-stars.html
Shirikisho la Soka la Tanzania(TFF) linataraji kusaini mkataba na kampuni ya Serengeti Breweries(SBL) wa kuidhamini upya wa Taifa Stars leo jioni.
Serengeti inachukua kijiti kutoka kwa Tanzania Breweries (TBL) iliyomaliza mkataba wake na TFF mwishoni mwa mwaka jana.
Ingawa taarifa za awali zinadai kwamba mwenendo wa Stars katika miaka ya hivi karibuni haukuwaridhisha TBL.