Rodriguez avurugwa Real Madrid






 Kocha Jose Pekerman amesema kitendo cha uongozi wa Real Madrid kutomkubali James Rodriguez licha ya kuonyesha kiwango cha juu, kimemvuruga mchezaji huyo.
Hata hivyo, mchezaji huyo raia wa Columbia, kocha wa timu yake ya Taifa, Pekerman amekuwa akimwamini, lakini ameshangazwa kutopewa kipaumbele kwenye klabu yake.
Mchezaji huyo ameonekana kutopewa kipaumbele kwenye kikosi hicho cha Santiago Bernabeu, huku akikosekana kwenye kikosi kilichocheza fainali ya Ligi ya Mabingwa wiki iliyopita.
Kiungo huyo mwenye miaka 25 alitua Madrid akitokea Monaco mwaka 2014  pia kumekuwapo taarifa za kuhamia Manchester United, lakini mchezaji huyo anaonekana kutokukubalika Ulaya. 

Related

michezo na burudani 1424366660214633177

Post a Comment

emo-but-icon

item
Kicbjamii