Mahakama yaamuru Seth kutibiwa Muhimbili




Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeamuru mmiliki wa Kampuni ya Kufua Umeme ya IPTL, Habinder Sethi, kwenda kutibiwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH).
Uamuzi huo umetolewa leo Jumatano Machi 28, 2018  na Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo,  Huruma Shaidi baada ya mshtakiwa huyo kujieleza mahakamani hapo kuwa afya yake siyo  nzuri  hivyo anaomba kupelekwa hospitali kwa ajili ya matibabu.
"Mshtakiwa anaonekana hata kwa macho,  hivyo naamuru mshtakiwa huyu apelekwe Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, akapatiwe matibabu ili kesi yake itakavyokuja kuendelea awe na afya nzuri ," amesema hakimu Shahidi.
Mbali na Seth,  mshtakiwa mwingine katika kesi hiyo ni mfanyabiashara, James Rugemarila  ambao kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka 12 katika Mahakama hiyo.
Awali wakili wa Takukuru,  Pendo Temu akisaidiana na Leonard Swai  alidai mahakamani hapo kuwa kesi hiyo ilikuja kwa ajili ya kutajwa na upelelezi wa shauri bado haujakamilika.
Katika kesi ya msingi,  washtakiwa kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka 12 ya uhujumu uchumi, utakatisha fedha na kuisababisha Serikali hasara ya Sh309 bilioni.

Related

kitaifa 8932733139036592960

Post a Comment

emo-but-icon

item
Kicbjamii