Freeman Mbowe aachiwa usiku ‘mnene’




Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe 

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe ameachiwa saa saba na robo usiku wa kuamkia leo baada ya kuhojiwa na Jeshi la Polisi.
Mbowe alikamatwa jana Jumatatu jioni wakati akienda kujisalimisha polisi na kupekuliwa nyumbani kwake kabla ya kuhojiwa hadi alipoachiwa usiku.
Ofisa habari wa chama hicho, Tumaini Makene ameithibitishia Mwananchi Digital taarifa za kuachiwa mwanasiasa huyo kuwa ni za kweli.
Hata hivyo, taarifa iliyosambazwa na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Salum Mwalimu kupitia mitandao ya kijamii imesema kuwa chama hicho kitatoa taarifa zaidi juu ya tukio hilo leo.
“Tunawashukuru wote kwa sala, maombi na subira na hivyo kuhitimisha salama saa kumi za mwenyekiti wetu kuwa chini ya Jeshi la Polisi katika Kituo Kikuu cha Polisi, Dar es Salaam,” Mwalimu amesema.

Related

siasa 5105709186776017910

Post a Comment

emo-but-icon

item
Kicbjamii