Banda ajitangaza kuikacha Simba na kujiunga na Baroka FC ya Sauzi

Beki wa Simba, Abdi Banda amefichuka siri kuwa mbioni kujiunga na klabu ya Baroka FC inayoshiriki Ligi Kuu Afrika Kusini (PLS).
Banda amemaliza mkataba wake na Simba mwezi uliopita alitangaza kuondoka kwenye timu hiyo kabla ya mchezo wa fainali ya Kombe la Shirikisho dhidi ya Mbao mwishoni mwa mwezi  wa Mei mwaka huu.
Hata hivyo, uongozi wa Simba ulikaa naye na kufanya mazungumzo yaliyofanikisha adhma yake ya kusaini mkataba na timu hiyo, lakini kwa sharti kwamba akipata timu yoyote wakati wowote ataondoka.
Wakati taarifa zikidai hakuwa amesaini mkataba  huo wakati anaondoka na timu ya Taifa Stars kushiriki mashindano ya Cosafa imezua  sintofahamu juu ya beki huyo kufichua kuwa  atakuwa mchezaji wa Baroka FC  msimu ujao.
Banda alitumia akaunti yake Instagram  kuthibitisha kwamba kwa sasa ni mchezaji mpya wa Baroka.
Endapo atajiunga na timu hiyo Banda atakuwa  amefuata nyayo za wachezaji wawili wa ukanda  huu wa Afrika Mashariki kuichezea timu hiyo  wengeni ni Khalid Aucho wa Kenya na Geffrey Massa wa Uganda.

Related

michezo na burudani 8017587191695915484

Post a Comment

emo-but-icon

item
Kicbjamii