Vituo vya mafuta kuendelea kufungwa





Vituo kadhaa vya kuuza  dizeli, petroli na mafuta ya taa vimefungwa nchi nzima kutokana na kutokuwa na mashine za kielektroniki za kutoa risiti (EFDs).
Hatua hiyo inayotekelezwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), imeelezwa kuwaathiri si tu wenye vituo bali hata watumiaji.
Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi wa TRARichard Kayombo amesema leo  Julai 14 na kuongeza kwamba  wanaendelea na kazi hiyo nchi nzima ili kuhakikisha sheria inatekelezwa.

Related

uchumi na biashara 3977222006619333066

Post a Comment

emo-but-icon

item
Kicbjamii